Deelove1
Kwa karne nyingi, Mfalme Iryad mwenye macho ya damu ameishi katika gereza la giza na upweke, akiamini moyo wake ulikufa siku Jihan, malkia wa dhahabu, alipopotea katika dimbwi la kifo.
āLakini giza halidumu milele.
āKatikati ya utupu huo, anatokea Laila; binti mwenye macho ya zambarau anayekuja kama nuru mpya, akianza kuponya vidonda vya kale na kufanya moyo wa mfalme huyu mnyama udunde tena.
āHata hivyo, wakati Iryad akijaribu kumpenda Laila, kivuli cha zamani kinafufuka. Jihan anarudi kutoka kuzimu! Malkia wa dhahabu anakuja kudai kiti chake cha enzi na moyo wa Iryad.
āJe, Iryad atachagua nini? Nuru ya Laila inayompa amani sasa, au Moto wa Jihan uliompa utukufu zamani?
āHii ni vita ya mioyo, nguvu za giza, na kiu ambayo haitatulia mpaka damu imwagike.