Wacha nkawasimlie ngano
Walakini si ngano ni hadithi
Maanake mimi ni muhusika
Katika hii hadithiKunaye huyu bwana mmoja
Aliyenunua pande la shamba langu
Basi bwana huyo ni bwenyenye
Magari barazani
Ua la mawe
Jumba la kufahari
Na kisha bango
" MBWA KALI "si mimi si mke wangu si watoto wangu
Tunaweza ingia kwenye hili kasri
Ingawa alikojenga bwana huyu
Wakati mmoja tulipaita kwetu
Ila sasa sisi wageni tuHaya yote si hoja
Ya mno ni haya
Watoto wangu hawatacheza
Maanake wanatifua vumbi ikatwaa madirishani pake
Makelele ya wanangu chukizo
Eti mama mkubwa abarizi barazaniNa ukidhani mwisho hii lele tu
Jana nimewapata wanangu wakila uani
Kuuliza mbona, maanake si kawaida
Kitoweo cha nyama walinyimwa
Bahati nzuri harufu uani yafikaMaskini mimi nii hoi
Miliki yangu ni baiskeli kuu kuu
Ambayo nikaridhi kwa babu
Zaidi sina
Nifanyeje maanake masaibu sasa wimbo
Tangia nimpate jirani tajiri
Walau ningekuwa nimepangisha
Basi ningehama, lakini huku kwangu!
![](https://img.wattpad.com/cover/152370035-288-k412920.jpg)