Leo itakapokuwa jana
Na jana kuwa juzi
Juzi itasahaulika
Na mengi tuliyoyafanya pamoja
Ni bayana kuwa tutayasahau
Mwanzo tutakumbukana
Utanikumbuka kwa moyo legevu
Wenye chembechembe za mseto wa hisia
Lakini jinsi ambavyo siku zinapozidi kuyoyoma
Mahaba yako bila shaka sharti yatasalimu amri
Na utanisahau na yote hayo yatapita
Mwenzio uendako sifahamu
Safari yako ya mbali ishang'oa nanga
Nami sina budi ila kukuaga na majonzi moyoni
Kwa kuwa hatima yako mwenzio si kafu yangu
Laazizi mema usio kifani nakutakiya
Maisha mazuri yenye amani na mafanikio
Ndiyo furaha yangu kwako ewe mpenzi
Siku zako zitawaliwe na siha njema laazizi
Naweka wazi shahidi moyo wangu
Umeniwacha na donda
Asilani lisilo na tiba
Ila natumai nami siku moja
Nitampata mwandani wangu
Awe fundi wa raha zangu
Na mpenzi wa roho yangu
Na siku zikiruhusu sisi kukutana
Nitakusalimu na bashasha usoni
Kwa kuwa sina kinyongo nawe mpenzi
Nenda salama laazizi
Jalali akujaliye mazuri uyatafutayo
YOU ARE READING
My Unknown Lover
PoetryWe break up just to make up, this won't be our first time it could be the second or our third time but its not the last time. You said some things I said some things too. I hurt your feelings and you hurt mine and I dont know what is worse. Even the...
